Sunday, June 9, 2013

FUATILIA STORI HII YENYE UHALISIA WASASA WA SIASA ZA TANZANIA KATIKA CHAMA FULANI KUELEKEA 2015...

PRESIDENTIAL PREPARATION   - 2
Piiiiiiiiiiiiiiiii,piiiiiiiiiiiiiiiiii,piiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii, ilikuwa ni honi ya gari inapigwa getini kwa mheshimiwa Leornard, na kumfanya mlinzi aende kuchungulia  nani alikuwa anapiga honi  getini. Lakini wakati baba askofu anafika getini kwa mheshimiwa Leornard tayari Alisha mtaarifu kama kafika, wakati mlinzi anachungulia getini, simu yake  ya kibandani iliita na alipoipokea, aliambiwa na mheshimiwa Leornard amfungulie baba askofu. Mlinzi alirudi getini na kumfungulia Baba Askofu. Baada ya kuingia ndani Baba askofu aliegesha gari yake , sehemu ya maegesho ya magari nyumbani kwa mheshimiwa
Leornard na alipo shuka kutoka kwenye gari alimsalimia askari Yule wa getini. Na baada ya salamu askari Yule alimuongoza Baba Askofu mpaka alipokuwa amekaa mheshimiwa Leornard  na Mzee Anthony.
Mheshimiwa Leornard: Oooooh Baba Askofu karibu sana.

Baba Askofu: Asante sana, tumsifu yesu kristo. Mheshimiwa Leornard kwa pamoja na Mzee Anthony: waliitikia milele amina.

Baada ya kujuliana hali za majumbani mwao wote watatu kwa pamoja, Silyvia mfanyakazi wa nyumbani kwa mheshimiwa Leornard alifika na kumsalimu baba askofu, na kumuuliza kinywaji ambacho angependa kutumia, kipindi hicho mheshimiwa na mzee wa kanisa mzee Anthony walikuwa wakiendelea kunywa juice na baba askofu aliomba aletewe maji ya kunywa ili aweze kupooza koo. Baada ya muda mfupi mama Lawrence, mke wa mheshimiwa Leornard alitoka ndani akiwa na maji na kwenda kumuhudumia baba askofu, na kusalimiana kidogo na mama Lawrence alirudi ndani na kumuacha mheshimiwa Leonard, Baba Askofu pamoja na mzee Anthony wakiendelea na mazungumzo yao.

Mzee Anthony; aaaaah Baba Askofu, baada ya misa ya juzi kuona umezungumzia sana swala la michango na sadaka kwa ujumla kwa wauminii……….Baba Askofu: ndiyo ndiyo

Mzee Anthony: nilifikilia sana na kujiuliza maswali mengi ni kivipi kupitia tu sadaka tungeweza kumalizia ujenzi ambao umebakia, tena ambao ni mkubwa kuliko sehemu tuliyojenga, “ni kweli mzee wa kanisa” yalikuwa ni maneno yake baba askofu. Niliamua kumfuata Mheshimiwa Leornard hapa, nikamuelezea hali halisi juu ya sehemu ya ujenzi wa kanisa letu ulipofikia, na yeye kwa upande wake amehaidi kuchangia milioni 100 pesa za kitanzania. Abarikiwe na Mwenyezi Mungu atamlipa alisema baba askofu. Aliendelea mzee wa kanisa kwa kusema, lakini wakati tukiyazungumza haya, shemeji mama Lawrence naye alikuwepo na akashauri kwamba mheshimiwa Leonard ni mtu wa watu anayependwa sana na watu, kwahiyo ingekuwa vyema ahudhurie ibada na kufanya harambee  kwa waumini ili tukamilishe ujenzi wa nyumba ya ibada, naimani waumini wataweza kumsikiliza kiongozi wao kwasababu wanampenda na wanaweza kumalizia kiasi kilichobaki.

Baba Askofu : Ashukuriwe Mwenyezi Mungu kwa kila jambo, wazo zuri sana mzee wa kanisa, naimani haya yote ni mapenzi mema ya mwenyezi Mungu juu ya nyumba yake ya ibada. “nikweli baba askofu ”alisema mheshimiwa Leornard. Karibu sanamheshimiwa Leonard kanisani kwetu kwa ajili ya huduma za kiroho na kuwahamasisha waumini juu ya ujenzi wa nyumba yao ya ibada.

No comments: