![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgAYB0pnKs-cZHzm-_EWgkoRXEIVy32hzU9jeoSjE-M2eeviTwnOn4V6j636VRK3rHS-APdtiUPdjewz35EFvrdsCUOqNwmTFhIxo-wkulzcIXBjEDFkadTUwJVXEwfdsewY1QpP7VMT-Tr/s1600/Arusha.jpg)
Monday, May 6, 2013
JESHI LA POLISI JIJINI ARUSHA LIMETHIBITISHA KUTOKEA KWA VIFO VYA WATU WATATU NA WENGINE 61 KUJERUHIWA KUFUATIA MLIPUKO
Jeshi la Polisi jijini Arusha limethibitisha
kutokea kwa vifo vya watu watatu na wengine 61 kujeruhiwa kufuatia
mlipuko wa kitu kinachodaiwa kuwa ni bomu katika Kanisa la Mtakatifu
Yoseph Mfanyakazi Olasiti lililokuwa lizunduliwe na Balozi wa Vatican
nchini Tanzania Francis Kadida.
Mlipuko huo umetokea jana Majira ya saa
tano asubuhi ambapo mashuhuda wa tukio hilo akiwemo RICHARD KOPLO na
HILDA MASUWE wamedai kumuona mtu mmoja akitupa kitu kanisani hapo na
kukimbia huku akipiga kelele za mwizi. Kwa upande wake Kamanda wa Ploisi
wa Mkoa wa Arusha LIBERATUS SABAS amesema, kufuatia tukio hilo wameanza
uchunguzi kuwabaini waliohusika ili wachukuliwe hatua kali za kisheria.
Kwa ujumla tukio hilo la kushtukiza limegusa hisia za watu wengi, kwa
kuliona hilo Mkuu wa Arusha Magesa Mulongo anatoa wito kwa jamii kuwa na
subira na subira wakati Jeshi la Polisi likifanya uchunguzi kuwabaini
wanaohusika. Kufuatia hali hiyo Msaidizi wa Askofu Jimbo la Kaskazini
Padre TENGE amelazimika kuharisha uzinduzi wa Kanisa hilo Jipya lililo
chini ya Parokia ya Burka ili kuhakikisha usalama wa waumini na
majeruhi.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgAYB0pnKs-cZHzm-_EWgkoRXEIVy32hzU9jeoSjE-M2eeviTwnOn4V6j636VRK3rHS-APdtiUPdjewz35EFvrdsCUOqNwmTFhIxo-wkulzcIXBjEDFkadTUwJVXEwfdsewY1QpP7VMT-Tr/s1600/Arusha.jpg)
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment