Jose Mourinho atua rasmi Chelsea
This will be an emotional return of the ‘Special One’ to his special club and Chelsea supporters from all over the world must be highly thrilled after reading this news.ESPN has also reported the same story quoting The Sun.
Jose Mourinho is expected to join the squad at Stamford Bridge after his last game with Spanish side Real Madrid, this weekend.
The arrival of Jose Mourinho was always on the card and the rumor got current after Real Madrid announced that the Portuguese wizard will be terminated from his contract on a mutual agreement. Jose Mourinho was spotted in London last weekend and he was on the VIP stand watching the Wembley play-off.
Many of the internal Chelsea sources have also confirmed the arrival of Jose, stating that, “it’s official,Jose is a Chelsea man again’.'Everyone is delighted he is coming back-the club,player and fans’.
Most of the Chelsea players have already declared their dream to work under Jose Mourinho, including Fernando Torres, David Luiz, Lukaku,Courtois and Eden Hazard.
Rob Beasley on twitter wrote,” I am pleased to officially announce that Jose Mourinho signed a contract with Chelsea FC on Tuesday to be their new manager”.
Being a Chelsea supported I am also highly exited with this news and wish all the very best to Jose and Chelsea.
HUU NDIO UCHAMBUZI NA UTABIRI WANGU WA FAINALI YA BORRUSIA DORTMUND VS BAYERN MUNICH
FC Bayern wanakutana na mtihani
mgumu usiku wa leo watakapocheza dhidi ya Borussia Dortmund kwenye dimba
la Wembley jijini London. Leo ni siku ya kuondokana na mkosi mkubwa
unaowatawala mabavarians ambao ndio timu inayoongoza kwa kufungwa kwenye
UEFA Champiosn League - leo ni siku ya kufuta machungu kwa kupoteza
mechi ya fainali ya mwaka jana ambayo walistahili kushinda ingawa bahati
haikuwa upande wao.
Hii ni fainali ya kwanza ya wajerumani ambao wanastahili kuwemo kwenye fainali hiyo. Utakuwa mchezo mzuri wa kukumbukwa.
Baada ya kusemwa kuwa kutolewa kwenye
hatua ya makundi ya ligi ya mabingwa wa ulaya msimu wa 2011-12, Dortmund
hatimaye wameyachukulia umakini mashindano haya kwa gaharama ya
kupoteza ubingwa wa nyumbani.
Ingawa, mchezo wao kwenye Champions
League umekuwa wa aina yake. Nguvu, ushirikiano, mbinu za mchezo wao
zimekuwa nzuri kiasi cha kuvishinda vilabu kama Real Madrid.
Mario Götze, kiungo mchezashaji wao,
ataukosa mchezo huo kutokana na majeruhi ya misuli. Alijaribu kurudisha
fitness yake kupitia mazoezi, lakini bahati haikuwa yake na akaawambia
mchezo wake wa mwisho wa msimu huu ulikuwa pale Santiago Bernabeu. Ujuzi
ambao BVB wataukosa ni pasi muhimu, kukimbiza mpira na mashuti yenye
madhara
Wachezaji wa kuchungwa.
Robert Lewandowski amegeuka kuwa
mshambuliaji wa kiwango cha dunia, ameonyesha utulivu mbele ya lango la
adui ambao washambuliaji wanakosa. Ana control nzuri ya mpira, anapiga
mashuti yenye kulenga goli.
Muhimu zaidi, ni hazina ya Dortmund
kwenye kulinda lango - golikipa Roman Weidenfeller. Uwezo wake wa kudaka
uliinyima Bayern ushindi kwenye michezo kadhaa iliyopita msimu huu.
Beki wa kati Mats Hummels anaweza
akacheza mechi ya fainali pamoja na kuwa na majeruhi. Kitu cha kuvutia
kuhusu yeye ni kwamba pamoja na mlinzi kwa ujumla, lakini pia anaweza
akaigharimu timu yake kwa makosa ya kizembe.
Wakati uzuri wa Dortmund inacheza vizuri
hata bila kuwa na mpira, mchezo mzuri wa kupasiana unaweza ukawadhuru
kwenye nusu yao ya uwanja. Pia wana udhaifu mkubwa kwenye mipira mirefu.
Bayern, wanapaa kwenye muda muafaka
Majeruhi: Badstuber, Kroos.
Huu ni mchezo unaomaanisha kila kitu kwa Bayern, ambayo ipo kwenye kiwango cha juu kwenye muda sahihi.
The bavarians wapo kwenye moto safari
hii kwenye ulinzi na ushambuliaji. Udhaifu wao uliowagharimu msimu
uliopita ni nguvu ya akili, udhaifu ambao umeshashughulikiwa. Sasa hivi
wana ile hali ya winning mentallity - angalia namna walivyotoka nyuma na
kuwafunga Borrusia Monchengladbach 4-3.
Franck Ribéry yupo kwenye kiwango cha
dunia akicheza winga ya kushoto, unaweza ukasema hivyo pia kwa Thomas
Muller ambaye anashughulika na majukumu ya kushambulia aliyokuwa nayo
Toni Kroos.
Bastian Schweinsteiger na kila kitu cha
kutoa kwenye mchezo huu. Ni package iliyokamilika kama mchezaji, box to
box midle, yupo kwenye kiwango cha juu sana.
Uzuri wa Bayern hivi sasa mpaka
wachezaji ambao walikuwa wavivu kama Arjen Robben wanakaba, timu yote
inakaba kwa pamoja na wanashambulia kwa pamoja.
Ikiwa Bayern watacheza kwenye kiwango
cha juu usiku wa leo basi itawachukua BVB kutumia vipaji binafsi zaidi
vya wachezaji kuweza kushinda.
Vita binafsi leo hii itakuwa kati ya
winga wa kushoto wa Bayern Frank Ribery vs Lukasz Piszczek. Kwa spidi
aliyonayo Mpoland huyo, na uwezo wake wa kuzuia itamchukua uwezo mwingi
sana Frank Ribery kuweza kupita.
Mara ya mwisho Bayern wameifunga
Dortmund, walimtumia zaidi Toni Kroos na uwezo wake wa kumiliki mpira -
Muller hana uwezo mkubwa wa kukaa na mpira kama ilivyo kwa Kroos hivyo
mambo yanaweza magumu kiasi.
Utabiri wangu nawapa Bayern nafasi ya
kushinda. Mafunzo waliyoyapata miaka iliyopita hasa msimu uliopita dhidi
ya Chelsea yatawapa hali ya kupigana zaidi. Hata kama wataanza
kufungwa, watashindana na kuhakikisha safari hii wanaepukana na mkosi wa
fainali ya Champions League. Dortmund wana mtindo wa kupaniki - angalia
katika mechi ya pili dhidi ya Madrid nusura waondolewe pamoja kuwa
walikuwa na hazina ya mabao 4-0.
Vikosi vinavyoweza kuanza
FC Bayern (4-2-3-1)
Neuer – Lahm, Boateng, Dante, Alaba – Martinez, Schweinsteiger – Robben, Müller, Ribéry – Mandzukic
Borussia Dortmund (4-2-3-1)
Weidenfeller – Piszczek, Subotic, Hummels, Schmelzer – Gündogan, Kehl – Blaszczykowski, Reus, Grosskreutz – Lewandowski
Location: Wembley Stadium, London
Referee: Nicola Rizzoli (Italy)
source: Shafih dauda-london
No comments:
Post a Comment