Inawezekana Serikali ikawa haishtushwi na mchezo wa triple K, kisa hasa
ni kiburi cha kuwakumbatia mataifa makubwa mawili Duniani China na
Marekani, na kuthibitisha hilo viongozi hao wamekuwa na mbwembwe sana
kwa ziara zao zote walizofanya Africa, Wa Kiongozi wa China kufanya
ziara yake ya kwanza nje kuwa Tanzania na Marekani kutumia muda mwingi
tu ukilinganisha na nchi nyingine kufanya ziara Tanzania.
Kuna messages nyingi sana katika ziara za watu hawa. Bahati Mbaya sana
ukiungana na Mataifa haya huwa huwajibiki kwa waliokkupigia kura bali
unawajibika kwao, na hii ndio tofauti. Mambo mengi yanaweza yasiwe wazi
kwa kigezo cha usalama wa nchi husika. Ingawa mchezo inaoucheza
Tanzania na Mataifa haya makubwa mawili ni wa kutatansiha, lakini
yawezekana kabisa ikanufaika. Hofu yangu ni kuwa bado kabisa hatujaweza
kupenya vya kutosha kwenye masoko ya mataifa haya, na kwakuwa
hatuzalishi kiviwanda kiasi cha kutosha na kuobora unaohitajika katika
ushindani wa kimataifa, ni wazi tutategemea Kilimo kuexport. Hatari
yake ni kuwa kilimo hicho sio kule cha bibi na babu yangu au mjomba
wangu kule kijijini, ili tuweze kupata soko uwezekano mkubwa kwa kigezo
cha ubora na kiwango watakuja wenyewe kulima na kuuza, na sisi
tufaidike na kodi, ambayo kama hakutakuwa na Tax holiday basi itakuja
mapema, jambo ambalo sina uhakika nalo.
Soko kubwa na la uhakika ambalo hata Mwalimu alilizungumzia na
linaloweza kukuza uchumi kwa haraka ni soko la Afrika. Haya masoko
hayajali sana ubora wa bidhaa zetu na hawawezi kuweka vikwazo vikubwa
kiasi hicho labda kuwe na ushindani wa bidhaa za ndani na za nje ya
nchi husika. Kenya iliwahi kufaidika sana na soko la Tanzania miaka ya
80 na 90, kwa kuingiza bidhaa za plastiki, sabuni na vipodozi ikiwa ni
baadhi tu. Nadhani uhusiano wa triple K ni wa kuutizama kwa jicho a
husuda na kuona ni jinsi gani tutamudu ushindani huu hasa biashara ya
Bandari, na Reli ambayo tuliwahi kusikia Kagame na Museveni mara kadhaa
wakijaribu kutushawishi tuijenge ili waitumie kwa bandari ya Tanga na
Dar es Salaam. Wakati huo uhusiano wao na Kenya haukuwa mzuri sana.
Kijana Uhuru naona anajua hili na sasa anatumia loophole ya ukiritimba
wetu katika kukuza uchumi kutap opportunity ya kukuza biashara na chi
hizi. Tusisahau tayari soko lao sasa linaenea Ethiopia na Sudani ya
Kusini na hivi punde itakuwa Somalia, ni soko kubwa sana lenye walaji
wengi tu ukilinganisha na majirani wetu wa kusini wa Zambia, Malawi na
Msumbiji. Angalau Kongo tunaitegemea, na kama tutashinda vita kama
walivyofanya Kenya.
Uhusiano wetu na Kenya na Rwanda umeingia doa kwa sababu kubwa mbili.
Kwanza kuingia katika vita ya Kongo tayari kumemuudhi sana Kagame,
ambaye ni rafiki ndugu wa Museveni kwa mengi tu. Uhusiano wetu na
mataifa ya Magharibi unatudhibiti sisi kuikumbatia Kenya ambayo
kiongozi wake ni mshtakiwa katika Mahakama ya Kimataifa. Watatu hawa
wanalijua hili na kauli ya JK ilitia msumari wa moto kwenye kidonda
kibichi cha Kagame na Uhuru.
Ni pale ambapo tutapata Kiongozi mpya baada ya uchaguzi na ambaye ana
siasa zisizofungamana na upande wowote na ambaye anajali uchumi zaidi
kuliko Siasa, ndipo tutashuhudia mabadiliko. Kwa sasa kiongozi wetu
anasimamia Siasa zaidi katika kukuza uchumi na hilo anaonekana
kufanikiwa ingawa wachunguzi wa mambo tayari wanamkosoa kwa kukumbatia
siasa na matabaka kimyakimya bila kuwa muwazi kama kiongozi katika kutoa
muelekeo wa mambo ya Kitaifa. Anachukuliwa kuwa mtu mwenye kupuuzia
mambo mengi nyeti yanayoathiri Siasa na Uchumi wa nchi mpaka pae
yanapokuwa ya moto, mtu ambaye yawezekana akawa hapendi kulaumiwa kwa
jambo lolote.
Wasiwasi mkubwa na kuwa kila wanapofika viongozi wa mataifa haya
makubwa Duniani wanasaini Mikataba kedekede, ambayo wananchi wengi
hawajashiriki na aghalabu inajulikana undani wake. Je ujio huu na
kusainiwa kwa mikataba hii hakutaathiri muelekeo wa kiuchumi na
kisisasa wa miaka ijayo hata kama JK akiwa hayupo madarakani? Je ni
mipango yenye nia njema ya muda mrefu au ni kama ile ya kupofusha macho
na tuanpokuja kujua tunakuwa tumechelewa? Hatujui, maswali haya
yatajibiwa tu na kauli za JK katika hotuba zijazo na kutueleza
kinagaubaga nini anachokifanya sasa kwa lugha nyepesi huku akitambua
kuwa anawajibika kwetu na si kwa wangine.
;source profesa.
No comments:
Post a Comment