Thursday, June 6, 2013

FUATILIA STORI HII YENYE UHALISIA WASASA WA SIASA ZA TANZANIA KATIKA CHAMA FULANI KUELEKEA 2015...



PRESIDENTIAL PREPARATION  -1
#################################################################################

Ndani ya siku chache zijazo chama chetu kitakamilisha chaguzi zake za ndani, zoezi ambalo limechukua takribani mwaka mzima, tangu chaguzi za kwenye mashina zilipoanza. Zoezi hili litakapo kamilika katika mkutano mkuu wa chama chetu, chombo ambacho ni cha juu kabisa cha maamuzi ndani ya chama chetu, kitakuwa na uongozi mpya katika nafasi zote.
Kutakuwepo na viongozi wapya kabisa, watakuwepo na waliorudi na wapo ambao watakuwa wamebadilishwa nafasi zao. Wapo wale ambao licha ya kujaribu sana watakuwa wametupwa kwenye nafasi za uongozi ndani ya chama hata kama wanazo nafasi zao za kiserikali.
Viongozi hawa wapya watakao chaguliwandio watakao kuwa wajumbe wa mkutano mkuu wa chama chetu,


mkutano mkuu wa chama ndicho chombo cha juu kabisa cha maamuzi ndani ya chama chetu, upo juu ya vyombo vingine vyote , ikiwemo katiba ya chama chetu, kwani ndicho chombo ambacho kinaweza kubadili katiba ya chama bila kuwa na rufaa dhidi yake. Lakini zaidi ni mkutano mkuu ndio ambao unaweza kutengua uamuzi wowote uliowahi kutolewa kipindi cha nyuma na chombo chochote au na mtu yeyote wa chama chetu. Kimsingi mkutano mkuu unaweza kutengua maamuzi ya sekretarieti ya chama au hata ya mwenyekiti wa chama chetu.
Kwahiyo kuelekea uchaguzi huu mkuu lazima kambi yetu ijipange kuhakikisha sekritarieti yote ya chama inatuunga mkono na theluthi mbili ya wajumbe wote wa mkutano mkuu wanakuwa ni wakambi yetu ndani ya chama.
Kwasababu kuelekea uchaguzi mkuu mara baada ya uchaguzi ndani ya chama  chetu ni lazima tutashuhudia kuibuka angalau kwa kambi mbili zaidi, ukiondoa kambi yetu ya mheshimiwa Leornard. Kambi  hizi mbili za ziadazitasabisha msuguano ndani ya chama chetu, kama tulivyo shuhudia katika uchaguzi mkuu wa nchi uliopita. Japokuwa uwezekano mkubwa wa kambi moja kati ya hizi mbili kujitoa ndani ya chama chetu . Hili litategemea jambo moja kubwa, kupatana kwa mheshimiwa Leonard na kambi ya mheshimiwa Seba, endapo tutashuhudia viongozi wetu hawa wakiamua kupatana na hatimaye kusimama pamoja, basi mgombea wa chama chetu ambaye atakuwa ni mheshimiwa Leonard atashinda kwa kishindo katika uchaguzi mkuu wa nchi ujao.

Lakini ukweli ni  kwamba majeraha ya kashifa ya ufisadi hayawezi kuponyeka kwa kukumbatiana au kwa kupiga picha pamoja, majeraha haya kwa mheshimiwa Leonard yamezama sana kiasi kwamba sioni uwezekano wowote wa kambi za chama chetu kuweza kukaa pamoja, ni lazima mwenye nguvu apishwe na atakapopita wanaobakia ni lazima watoke.

Written by: Lincoln Pascal 2012.
Don't miss every Thursday and Monday.
#####################################################################################

No comments: